Thursday, June 18, 2015

Manchester United yakomaa na Raphael Varane.

Club ya Manchester United bado inaendelea kumfukuzia beki wa Real Madrid, Raphael Varane ambaye Manchester United wamekuwa wakimtaka kumsajili kutoka Real Madrid.

Licha ya Real Madrid kukataa kmuachia Varane kwenda Manchester United lakini bado Manchester United  wanataka kumchukua beki huyo wa club ya Real Madrid. Gazeti la Express la nchini Uingereza limesema kwamba Manchester United inaweza ikamchukua Raphael Varane kutoka Real Madrid indapo tu Real Madrid ikikubali kumuachia beki huyo. Manchester United bado inaendelea kuishawishi Real Madrid ikubali dau la Club hiyo juu ya usajili wa Karim Benzema pamoja na Raphael Varane.

No comments:

Post a Comment