Tuesday, June 16, 2015

Fabric Muamba amshauri Harry Kane abaki Tottenham Hotspurs.

Mchezaji wa zamani wa club ya Arsenal, Birmingham City na club ya Bolton Wanderers Fabric Ndala Muamba ambaye kwa sasa amestaafu soccer, Fabric Muamba amemshauli mchezaji wa club ya Tottenham Hotspurs, Harry Kane aendelee kubaki katika club hiyo.

Muamba amesema hayo baada ya kutokea uvumi kuwa club ya Manchester United ipo mbioni kumsajili Harry Kane kutoka Tottenham. Fabric Muamba alisema hayo katika gazeti la Express ambapo Muamba alimshauri Harry Kane kutokuhiama Tottenham na kwenda Manchester United.

Harry Kane mwenye umri wa miaka 22 ambaye aliweza kufanya vizuri sana katika msimu uliomalizika kwa kuweza kushika nafasi ya pili katika orodha ya wachezaji wanaoongoza kwa magoli katika ligi ya EPL nchini Uingereza. Kane alimaliza ligi kwa idadi ya mabao zaidi ya 20 akiongozwa na mshambuliaji wa club ya Manchester City, Sergio Arguero aliyefunga mabao 23 katika msimu uliopita. Kane ambaye ameweza kufanya vizuri sana msimu uliopita hali iliofanya vilabu kadhaa vikitaka kumsajili mshambuliaji huyo wa Tottenham ambapo club ya Manchester United ikitaka kumsajili Harry Kane lakini Fabric Muamba ametoa ushauri kwa Harry Kane yakumtaka Kane aendelee kubaki katika club ya Tottenham hotspurs.



No comments:

Post a Comment